INAKARIBIA miezi miwili sasa tangu klabu ya soka ya nchini Ukraine Shaktar Donetsk kufanya mabadiliko kwenye benchi lao la ufundi kwa kumfukuza mwalimu Patrick Van Leeuwen na mikoba yake kupewa Marino Pusic (52) kukinoa kikosi hicho mpaka mwaka 2025-2026.

Tangu kufanyika kwa mabadiliko ya benchi la ufundi kijana wa Kitanzania ambaye alifanya vizuri sana kwenye michezo kadhaa aliyopewa nafasi ya kucheza, hapa namzungumzia Novatus Miroshi Dismas ambaye kwa sasa hana tena nafasi katika kikosi hicho na muda mwingi anakalia ubao.

Hata hivyo watu wengi wamekuwa wakijiuliza ni kwanini Novatus anakaa sana benchi, Je hana uwezo? au mabadiliko ya benchi la ufundi ni sababu ya kijana huyu kutopata nafasi?

Kwa mujibu wa Mwandishi wa Habari Nchini Ukraine amenukuliwa akisema kwamba "Sitaki kuamini kama sababu ni uwezo wake lakini kitendo cha Novatus kwenda hapo kwa mkopo akitokea Zulte naamini kuna hofu ya Shaktar kuendelea kumtumia kwakuwa wanahofia kumuweka kwenye njia ya kununuliwa na timu nyingine, kitu ambacho wao Shaktar hawanufaiki na chochote"

Kisha akamalizia kwa kusema "Ulaya vinaenda tofauti sana watu wanaangalia pesa kwanza"

Unaweza kufanya biashara yenye faida kubwa kwa mtaji mdogo wa kuanzia Tsh 200/= ukicheza michezo ya kasino ya mtandaoni ya MERIDIANBET, kubashiri soka kwa odds kubwa.

Kitu cha msingi hapa ni kuelewa kwamba Shaktar Donetsk ni miongoni mwa vilabu vinavyouza wachezaji kwenye timu nyingi Ulaya, ukiachana na klabu kama Ajax, Brighton, Tottenham, Sporting Lisbon, Dortmund nk.

Sambamba na hilo MERIDIANBET pia ndiyo chimbo pekee la maokoto kwa hapa Tanzania, bashiri mechi nyingi kwa odds kubwa, cheza michezo ya sloti na kasino ya mtandaoni uwe moja kati ya washindi wa kila siku.

NB: Meridianbet ukijisajiri tu unapata bonasi kibao za kasino ya mtandaoni na pia kila mechi inatoa odds kubwa PIGA *149*10# AU tembelea tovuti yao meridianbet.co.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...