Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania ( TPA) imezindua Rasmi Ofisi yake katika nchi ya Malawi ikiwa ni hatua ya Mamlaka hiyo kusogeza huduma za Bandari karibu na wateja wake wa nchini humo.

Waziri wa Uchukuzi wa Tanzania Mhe. Profesa Makame Mbarawa amesema, ofisi hiyo itapunguza usumbufu kwa wateja wa Bandari ya Dar es salaam kutoka nchini Malawi na watapata huduma zote wakiwa nchini mwao.

Kwa upande wake waziri wa Uchukuzi na ujenzi wa Malawi Mhe. Jacob Hara amesema, ofisi hiyo itakuwa na manufaa makubwa kwa wafanyabiashara wa Malawi na itarahisisha shughuli za usafirishaji wa mizigo kupitia bandari hiyo.

Mkurugenzi Mkuu wa TPA Bw. Plasduce Mbossa amesema uzinduzi wa ofisi hiyo unatimiza dhamira wa mamlaka hiyo kusogeza huduma zake kwa wateja wake.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...