Mkuu wa Polisi, Kitengo cha Dawati la Jinsia kata ya Kawe, ASP Elizabeth Msabira, akitoa zawadi kwa wanafunzi waliojibu vizuri wakati wa mafunzo ya elimu ya kupinga vitendo vya ukatili katika shule ya msingi Tumaini.

Wanafunzi wa shule ya sekondari Uhamiaji iliyopo Kurasini jijini Dar es Salaam wakiwa katika somo la utambuzi wa vitendo vya ukatili wa kijinsia.
Wakufunzi wa mafunzo hayo wakifuatilia matukio wakati wa uzinduzi wilayani Temeke katika shule ya msingi Mgulani.
Wanafunzi wa shule ya Mgulani wakisikiliza elimu ya utambuzi wa ukatili wa kijinsia inayotolewa na Maofisa kutoka madawati ya jinsia ya Jeshi la Polisi.
Wanafunzi kutoka baadhi ya shule za sekondari na msingi katika mkoa wa Dar es Salaam wanaendelea kunufaika kwa kupatiwa elimu ya kupinga vitendo vya ukatili wa Kijinsia na utambuzi wa vitendo hiyo, inayotolewa na Jeshi la Polisi, kwa udhamini wa kampuni ya Barrick, ikiwa ni maadhimisho ya siku 16 za kupinga vitendo vya ukatili wa kijinsia yanayoendelea.

Shule ambazo Maofisa kutoka madawati ya kijinsia ya Jeshi la Polisi tayari wamefikisha elimu hiyo ni shule ya msingi Tumaini Kawe, Mbezi Beach, Mgulani na Sekondari za Daniel Chongolo na Uhamiaji. Mafunzo haya yataendelea kufikia shule mbalimbali za msingi na sekondari na kwenye jamii zenye mikusanyiko ya watu wengi kwenye kipindi hiki cha maadhimisho hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...