Na Issa Mwadangala

MAOFISA Wakaguzi na Askari wa vyeo mbalimbali Mkoa wa Songwe wametakiwa kuendelea kujenga ushirikiano na wananchi na kutoa huduma bora ili kujenga imani kwa Wananchi wanaowahudumia.

Kauli hiyo imetolewa na Kamanda wa Poisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi wa Polisi ACP Theopista Mallya wakati alipofanya baraza na askari wa Mkoa huo Januari 10, 2024 wilayani Mbozi ikiwa ni kufanya tathimini na kuweka mkakati hususani kipindi hiki cha mwaka mpya wa 2024.

Kamanda Mallya pia aliwataka askari Polisi wanapotekeleza majukumu yao kuzingatia weledi na uadilifu ili kuleta matokeo chanya ndani ya Jeshi la Polisi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...