Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Taifa Balozi Dkt. Emanuel Nchimbi amewahakikishia Makatibu Wakuu wa Vyama Sita vya Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika kwamba Chama Cha Mapinduzi kina uhakika wa kushinda kwa kishindo katika changuzi za mwaka huu na mwaka kesho, kwa maana ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2025.

Dkt. Nchimbi ametoa kauli hiyo wakati akifungua kikao cha Makatibu Wakuu wa Vyama Sita vya Ukombozi wa Nchi za Kusini mwa Afrika kilichofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, iliyopo Kibaha mkoani Pwani.

Kauli hiyo aliitoa baada ya kuwapongeza Chama Cha ZANU - PF cha Zimbabwe Kwa kuibuka na ushindi katika uchaguzi wao walioufanya huku akivitakia pia heri ya ushindi NAMIBIA NA AFRIKA KUSINI kwenye uchaguzi wao mkuu ambao wao wanaufanya baadae mwaka huu na ANC cha Afrika kusini ambacho kimesheherekea kumbukumbu ya miaka 112 tangu kuanzishwa kwake.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...