Akizungumza na walimu na Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Nyamilama Mkuu wa wilaya ya Kwimba Mkoani Mwanza,Ng' wilabuzu Ludigija amesema serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imefanya kazi kubwa sana kwa kuweka mazingira wezeshi na rafiki katika upatikanaji wa elimu ikiwemo ujenzi wa madarasa ya kisasa.
Amewaomba wazazi na walezi kuunga mkono maendeleo hayo wananchi hawana budi kuwaruhusu watoto kuripoti shuleni na kuanza masomo mara moja ili kutengeneza kizazi cha uelewa kwani wanafunzi wa leo ndiyo viongozi wa baadaye.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...