Na John Walter -Babati

Mkuu wa wilaya ya Babati Lazaro Twange ameuagiza uongozi wa kijiji cha Galapo kuwalipa akina mama wanaojishughulisha na upondaji wa kokoto fedha wanazodai ifikapo siku ya Jumatatu Februari 26,2024.


Kina mama hao wamemwambia mkuu wa wilaya kwamba walifanya kazi hiyo kwa ajili ya ujenzi wa shule ya Msingi Galapo ambapo mpaka sasa hawajalipwa fedha wanazodai zaidi ya shilingi Milioni moja.


Mkuu wa wilaya ya Babati Lazaro Twange ameendelea na ziara ya kikazi katika Kata za wilaya hiyo kufanya mikutano ya hadhara kusikiliza na kutatua kero za Wananchi.
Akiwa kata ya Galapo, Twange amewataka wenyeviti wa vijiji,vitongoji na watendaji kuwahudumia wananchi kwa mujibu wa utaratibu ili kuepuka kero na migogoro na hatimaye kuwa na Maendeleo.


Katika ziara yake mkuu wa wilaya ameambatana na taasisi za serikali na watalaamu wengine ili kujibu kero husika.


 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...