Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, leo Jumamosi Februari 3, 2024, amemtembelea na kumjulia hali Ndugu Loth Lazaro Olemeirut, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Rorya, Mkoa wa Mara, ambaye amelazwa kwa ajili ya matibabu katika Hospitali ya Taifa Muhimbili – Mloganzila, jijini Dar Es Salaam. Kushoto ni Daktari Bingwa, Elineema Meda.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali Ndugu Loth Lazaro Olemeirut, Katibu wa CCM wa Wilaya ya Rorya, mkoani Mara, leo Jumamosi, Februari 3, 2024, ambaye amelazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili – Mloganzila, jijini Dar Es Salaam, kwa ajili ya matibabu. Kushoto ni Daktari Bingwa, Elineema Meda.
Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali Ndugu Peter Niboye, ambaye ni Kada wa CCM, anayeendelea ahueni akiwa nyumbani, jijini Dar Es Salaam, baada ya kutoka hospitali alikokuwa amelazwa hapo awali kwa ajili ya matibabu. Kushoto ni baba mzazi wa Peter, Mzee Josephat Niboye.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amemtembelea na kumjulia hali Ndugu Peter Niboye, ambaye ni Kada wa CCM, anayeendelea kupata ahueni akiwa nyumbani, jijini Dar Es Salaam, baada ya kutoka hospitali alikokuwa amelazwa hapo awali kwa ajili ya matibabu. Kushoto ni baba mzazi wa Peter, Mzee Josephat Niboye na kulia ni Bi. Edith Niboye, mama mzazi wa kada huyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...