Na Pamela Mollel,Chato

 Hifadhi ya Taifa ya Burigi -Chato, Sasa ipo tayari kupokea malfu ya watalii baada ya Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA) kukamilika miundombinu ya barabara na mawasiliano ambayo awali ilikuwa ni shida.

Hifadhi hii iliyonzishwa mwaka 2019 ,kiasi cha sh bilioni 3.3 tayari zimetumika kuimarisha miundombinu yake ili watalii wa ndani na nje waweze kutembelea .

Mkuu wa hifadhi hiyo, Kamishna Msaidizi Ismaili Omari akizungumza na waandishi wa habari za Utalii na Uhifadhi waliotembela hifadhi hiyo, alisema wanaalika watalii kutoka ndani na nje ya nchi kutembelea hifadhi hiyo.

" Shirika la hifadhi za Taifa (TANAPA ) limefanya maboresho makubwa ya Miundombinu na kazi inaendelea lakini pia Kampuni ya simu ya TTCL imeweka mnara wa Mawasiliano hifadhini" amesema.

Mhifadhi Omar alisema barabara zenye urefu wa kilomita 97.5 pamoja na madaraja na vivuko yamejengwa lakini pia sasa umekamilika ujenzi wa kambi za Utalii na makazi ya bei nafuu ya watalii ndani ya hifadhi .

"Lakini pia tunahifadhi mazingira na uoto wa asili na Sasa wanyamapori wameongezeka na wanaonekana kirahisi"amesem

Afisa utalii hifadhi ya Burigi- Chato ,Aldo Mduge amesema upekee wa hifadhi hiyo ni uwepo wa ndege aina ya Domo kiatu (African Shoebill) maziwa yanayo zunguka hifadhi wanyama wengi na ndege aina 400.

Mduge amesema hivi Sasa kuingia katika hifadhi hiyo ni rahisi kwa usafiri wa barabara,Anga na kupitia Maji .

"Awali kulikuwa na changamoto lakini Sasa hifadhi inafikika maeneo yote na tuna vivutio vingi ikiwepo wanyama wa kubwa kama Tembo,Simba,Chui,Nyati,Twiga na wengine "amesema

Akizungumzia makazi wa ndani ya hifadhi, Kaimu mkuu idara ya utalii hifadhi hiyo, Emmanuel Nyundo hiyo alisema uwekezaji walio ufanya ikiwemo kujenga kambi ya wageni ya kudumu huku akiwakaribisha wageni kuwekeza katika hifadhi hiyo kwani kuna maeneo mazuri.

"Kuna maeneo ya ujenzi wa kambi za Utalii,mahoteli na vivutio vingine vya Utalii"amesema

Hifadhi hii ina kilomita za mraba 4707 katika wilaya za Biharamulo,Chato,Karagwe ,Ngara na Muleba ipo katika mikoa ya Kagera na Geita.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...