Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ustawi na Maendeleo ya Jamii imeshauri Serikali iongeze bajeti ya Mfuko wa Maendeleo ya Vijana ili kufikia malengo na tija iliyokusudiwa ya kuwainua vijana kiuchumi.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Fatuma Toufiq (Mb) ametoa ushauri huo leo Februari 7, 2024 alipokuwa akiwasilisha taarifa ya kamati hiyo kuhusu shughuli za kamati kwa mwaka 2023.

Amesema kuwa, ufinyu wa bajeti umepelekea mfuko huo kushindwa kukidhi mahitaji ya utoaji mikopo kwa vijana.

Pia, Kamati imeshauri Serikali kuunganisha mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi ili kuwa na tija endelevu ya kuwezesha vijana kimitaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...