Na JANETH RAPHAEL - MichuziTv Dodoma


Wahudumu wa Mabasi ya Masafa Marefu Nchini watakiwa kutumia Weledi wa hali ya juu katika kutekeleza majukumu yao ili kupunguza malalamiko yaliyopo kutoka kwa wateja wao.

Rai hiyo imetolewa mapema leo Jijini Dodoma na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh Rosemary Senyamule katika ufunguzi wa mafunzo ya siku tano kwa Wahudumu wa Mabasi ya Masafa Marefu na Mijini yaliyofanyika Kikanda Jijini hapa Dodoma.

"Ni hakika,ikiwa kila Mmoja atatekeleza majukumu yake na kuyafanyia Kazi yote niliyotaja pamoja na mengineyo natumai kwamba malalamiko ya wateja wenu yatapungua. Ni muhimu kuzingatia yale mtakayojifunza ndani ya siku tano hapa,ili kuweza kufanikiwa ni lazima kila Mmoja wenu aweze kusoma na kufanya Kazi kwa Weledi wa hali ya juu".

"Hivyo nawaomba washiriki wa mafunzo haya kusoma kwa bidii mafunzo haya mtakayopata yakawaongezee tija katika vituo vyenu vya kazi. Ni Rai yangu kwenu kujituma katika mafunzo haya na kuwa wabunifu".

Aidha Mh Senyamule amesema kuwa kuwepo kwa mafunzo haya ni matokeo ya juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika mradi wa (EASTRIP.

"Ni dhahiri kuwa kuwepo kwa mafunzo haya ni matokeo ya juhudi za Serikali kupitia Wizara ya Uchukuzi, na Wizara ya Sayansi na Teknolojia waliowezesha kuwepo kwa mradi huu wa East Africa Skills For Transformation and Regional Intergration Project (EASTRIP)".

Naye Kaimu Makamu Mkuu wa Chuo cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) Dkt Prosper S. Nyaki ameeleza kuwa Kozi hii ni ya muda mfupi itawajengea uwezo a umahiri katika kuzitambua Sheria za LATRA na kanuni zake.

"Kozi hii ni ya muda mfupi itawajengea uwezo na umahiri katika kuzitambua Sheria za LATRA na kanuni zake,utoaji wa huduma Bora kwa wateja,mbinu za utoaji wa huduma za kwanza,usalama wa abiria na Mali zao, utunzaji wa mizigo na utambuzi wa bidhaa hatarishi,kwa kuzingatia kanuni za Usafirishaji,namna Bora ya kushughulikia Malalamiko ya wateja,usafi na utunzaji wa mazingira,mahusiano na Mawasiliano,nidhamu na unadhifu wa mtoa huduma,pamoja na marifa ya utoaji na umuhimu wa tiketi Mtandao".

Katika salamu zake Kaimu Mkuu wa chuo Mipango ya Maendeleo Vijini Dkt Godrich Mnyone amesema kuwa Nchi yetu sasahivi inachangamoto ya watoa huduma wa jamii hivyo watakapo maliza mafunzo haya wao wakalete majibu.

"Nchi yetu sasahivi Ina shida ya watoa huduma wa jamii hivyo ninyi mtakapomaliza mafunzo haya muende mkalete badiliko".

Akitoa Shukurani kwa niaba ya Wana Mafunzo wenzake Lameck James Haule ameahidu Mara baada ya mafunzo haya watakwenda kuwa wabunifu na kutangaza mazuri ya Serikali.

"Mimi niseme kwa niaba ya wenzangu baada ya mafunzo haya tutakuwa wabunifu na kutangaza mambo mazuri ya Serikali hasa katika Sekta ya usafirishaji".

Mafunzo haya ni ya siku tano, lakini bado kutakuwa a mafunzo mengine kama haya kwa wahudumu wa Mabasi kwa nyakati tofauti katika Kanda zote hapa Nchini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...