Zaidi ya Watumishi 100 wa Bohari ya Dawa (MSD) wanapatiwa mafunzo ya Mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma kwa Njia ya Mtandao (NeST). Mafunzo hayo yanayotolewa na Mamlaka ya udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) yanafanyika jijini Dar es Salaam kwa Siku Tano.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo Mkurugenzi Mkuu wa MSD Bw. Mavere Tukai amesema watumishi wa MSD wanapaswa kushiriki na kujifunza kikamilifu mfumo huu ili kuhakikisha mfumo unatatua changamoto mbalimbali za kiutendaji na kuleta tija katika upatikanaji wa bidhaa za afya nchini.

“ MSD tumewekeza sehemu kubwa katika kuhakikisha mfumo huu unakuwa na tija katika manunuzi ya bidhaa za afya. Tuna timu ambayo inafanyakazi na timu ya kitaifa inayotengeneza mfumo huu ili kuhakikisha unawezesha kwa ufasaha majukumu ya MSD”. Amesema Tukai.

Naye mkufunzi kutoka Mamlaka ya udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) Bw. Castor Claudius Komba - Meneja Mafunzo na Ushauri amesema lengo la mafunzo hayo ni kuhakikisha watumishi wa MSD wanakuwa na uelewa wa hali ya juu katika matumizi ya mfumo huo, kwani MSD ina majukumu nyeti ya kununua bidhaa za afya hivyo mfumo huu haupaswi kuwa kikwazo katika manunuzi ya bidhaa za afya nchini.

Pia Bw. Komba ameongeza kuwa anatarajia kuwa mfumo huo mpya utatatua changamoto zilizokuwepo wakati wa matumizi ya mfumo wa ununuzi wa Taneps.

Mafunzo haya ya Mfumo mpya wa Ununuzi wa Umma kwa Njia ya Mtandao (NeST) yanatolewa kwa siku tano kwa watumishi wa MSD wanaotoka Makao Makuu na Kanda za MSD.





 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...