Na; Mwandishi Wetu - DODOMA

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga amesema kuwa serikali imeendelea kuwezesha vijana wenye Ulemavu kupata mafunzo ya ukuzaji ujuzi na mikopo masharti nafuu ili kuboresha hali zao kimaisha.

Amesema hayo hii leo Februari 8, 2024 Bungeni, jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum Mhe. Mwantatu Khamis ambaye alitaka kujua vijana wenye Ulemavu wamenufaika vipi na mafunzo na mikopo inayotolewa na serikali.

Akijibu swali hilo, Mhe. Ummy Nderiananga amesema serikali inatekeleza mikakati na programu mbalimbali kwa lengo la kukuza ushiriki wa Watu wenye Ulemavu katika shughuli za kijamii, kisiasa na kiuchumi.

Ameongeza kuwa, kwa mwaka fedha 2022/23 zaidi ya vijana wenye Ulemavu wamenufaika na mafunzo ya ufundi stadi na marekebisho kupitia Programu ya Taifa ya Ukuzaji Ujuzi. Pia, kiasi cha mikopo Tsh. Bilioni 81.3 kimetolewa kwa wanufaika 640,723 ikiwemo Watu wenye Ulemavu ambayo imewasaidia kuanzisha na kuendeleza biashara zao.

Kwa upande mwengine, Mhe. Nderiananga ametoa wito kwa Watu wenye Ulemavu kuchangamkia fursa zinazotolewa na serikali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...