TUSIANDIKE HABARI ZINAZOWAVUNJA MOYO WANAMICHEZO WETU: WAZIRI NAPE

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Nape Moses Nnauye (Mb), amesema Serikali, kupitia Wizara anayoiongoza na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, itawezesha mafunzo ya ndani na nje ya nchi kwa waandishi wa habari za michezo kwa ajili ya fainali za AFCON 2027.

Akifungua TASWA Media Day Bonanza kwa niaba ya Waziri Mkuu, Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), katika viwanja vya Msasani Beach Club, Dar es Salaam, Februari 10, 2024, Waziri Nape alisema, 'Serikali kupitia Wizara ya Habari na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo tutandaa mafunzo pamoja na safari za nje ya nchi kwa waandishi wa habari za michezo ili kujiandaa vizuri katika kutoa habari za mashindano ya AFCON 2027.'

Aliongeza, 'Wanahabari ni watu muhimu katika kutangaza nchi yetu. Tunapenda kuwapa mafunzo na vifaa ili waweze kutangaza mashindano hayo kwa ufanisi.

Pia, nawasihi wanahabari wa michezo kufanya mazoezi ili kuhakikisha afya zao zinalindwa.'

Aidha, Waziri Nape aliwataka wanahabari kuepuka kuandika habari zinazowavunja moyo wanamichezo wa Tanzania, akisisitiza kuwa michezo ni mchanganyiko wa mafanikio na changamoto, hivyo ni muhimu kutoa msaada na uungwaji mkono kwa wanamichezo wetu.

"Tusiandike habari zinazowavunja moyo wanamichezo wetu," alisisitiza Waziri Nape, akitoa wito kwa waandishi wa habari za michezo.






Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...