Mhe Phaustine Kasike, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Msumbiji alikutana na Prof. Armindo Tiago, Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Msumbiji tarehe 20 Machi 2024 kwenye Ofisi za Wizara ya hiyo zilizopo Jijini Maputo.

Wakati wa Mkutano huo, Viongozi hao wawili walizungumza masuala mbalimbali ya Ushirikiano katika Sekta ya Afya ikiwemo pendekezo la kusainiwa Hati ya Makubaliano (MoU) itakayowezesha Tanzania kuuza Madawa na Vifaa Tiiba nchini Msumbiji.

Aidha, Viongozi hao walizungumza pendekezo la Tanzania la kutuma Timu ya Wataalam wa Afya watakaoweka kambi nchini Msumbiji kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wenye matatizo ya moyo.

Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania - Maputo

20 Machi, 2024



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...