Mhe Phaustine Kasike, Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania - Msumbiji alikutana na Prof. Armindo Tiago, Waziri wa Afya wa Jamhuri ya Msumbiji tarehe 20 Machi 2024 kwenye Ofisi za Wizara ya hiyo zilizopo Jijini Maputo.
Wakati wa Mkutano huo, Viongozi hao wawili walizungumza masuala mbalimbali ya Ushirikiano katika Sekta ya Afya ikiwemo pendekezo la kusainiwa Hati ya Makubaliano (MoU) itakayowezesha Tanzania kuuza Madawa na Vifaa Tiiba nchini Msumbiji.
Aidha, Viongozi hao walizungumza pendekezo la Tanzania la kutuma Timu ya Wataalam wa Afya watakaoweka kambi nchini Msumbiji kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wenye matatizo ya moyo.
Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania - Maputo
20 Machi, 2024



Wakati wa Mkutano huo, Viongozi hao wawili walizungumza masuala mbalimbali ya Ushirikiano katika Sekta ya Afya ikiwemo pendekezo la kusainiwa Hati ya Makubaliano (MoU) itakayowezesha Tanzania kuuza Madawa na Vifaa Tiiba nchini Msumbiji.
Aidha, Viongozi hao walizungumza pendekezo la Tanzania la kutuma Timu ya Wataalam wa Afya watakaoweka kambi nchini Msumbiji kwa ajili ya kutoa huduma kwa wananchi wenye matatizo ya moyo.
Imetolewa na Ubalozi wa Tanzania - Maputo
20 Machi, 2024




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...