Angela Msimbira, KAGERA

Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) imeitaka Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera kukamilisha utaratibu wa kupandishwa hadhi Zahanati ya Nshambya kuwa Hospitali ya Wilaya.

Maelekezo hayo yametolewa leo Machi 18,2024 na Makamu Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Staslaus Mabula alipokuwa akifanya majumuisho ya ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri hiyo.

Amesema Kamati imesikitishwa na ucheleweshaji wa upandishwaji hadhi ya zahanati hiyo tangu Mwaka 2021 licha serikali kujenga majengo sita ya kuongeza hadhi ya kuwa Hospitali.

"Inasikitisha sana kuona Halmashauri ya Manispaa ya bukoba hakuna watu wenye uchungu wa fedha zinazotolewa na serikali ambapo majengo yamejengwa 6 lakini linalotumika ni jengo la wagojwa waa nje tusuala hili halikubaliki hakikisheni hospitali hii inapata usajili na kitumike kama ilivyokusudiwa na Serikali, majengo yanatumika kwa matumizi yasiyokusudiwa kwa kuwa kwa sasa wanatoa huduma ngazi ya Zahanati wakati majengo yaliyopo ni ya Hospitali ya Wilaya,"amesema.

Aidha, amesema Kamati hiyo ina jukumu la kusimamia matumizi ya fedha za serikali za mitaa nchini hivyo wanakagua fedha zote zinazotolewa na serikali ili kuhakikidha zinatumika kwenye malengo yaliyokusudiwa na thamani halisi ya fedha ionekane.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...