Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi amejumuika na waumini wa dini ya Kiislamu na waombolezaji katika Dua ya khitma ya kumuombea aliyekuwa Rais wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Marehemu Mzee Ali Hassan Mwinyi ambayo inafanyika leo tarehe: 03 Machi 2024, katika viwanja vya maonesho Nyamanzi, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Dua hiyo imeandaliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kumuombea Marehemu Mzee Mwinyi ambaye amefariki dunia tarehe: 29 Februari 2024 katika hospitali ya Mzena, Dar es Salaam na kuzikwa tarehe: 02 Machi 2024 Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

Aidha, dua hiyo umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Chama, Dini na wananchi.











Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...