Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.
Baadhi ya miti ikivunwa katika shamba la miti Sao Hill wilaya ya Mufindi mkoani Iringa
Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.






Na Fredy Mgunda, Iringa.



SHAMBA la miti Sao Hill lililopo wilaya ya Mufindi mkoani Iringa huotesha miche milioni 5 ya miti kila mwaka katika bustani tatu zilizopo katika shamba hilo.




Akizungumza na waandishi wa habari Mhifadhi mkuu wa shamba la miti Sao Hill PCO Tebby Yoram alisema kuwa miche hiyo huoteshwa kwa ajili ya kupandwa katika shamba hilo na mingine kugaiwa wananchi,wadau na taasisi mbalimbali.




PCO Yoram alisema kuwa lengo la kubwa la kugawa miche hiyo ni kuendeleza uhifadhi wa misitu kwa wananchi na taasisi hizo kuendelea kupanda miti kwa wingi katika mashamba na kushiriki katika kuhifadhi shamba hilo.




Alisema kuwa kuelekea kilele cha siku ya upandaji miti kitaifa itakayofanyika katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro na uongozi wa shamba hilo umejipanga kupanda miti kwenye vyanzo vya maji vilivyopo katika shamba hilo.




PCO Yoram alisema kuwa wanapanda miti kwenye vyanzo vya maji kwa lengo la kuendelea kutunza vyanzo vya maji na shamba la miti Sao Hill hupanda hekta 2500 hadi hekta 300 kila mwaka.




Aidha PCO Yoram alisema kuwa licha ya kupanda miti mingi lakini shamba hilo huvunwa Laki 6 hadi 7 ujazo wa uvunaji wa mazao ya miti katika shamba hilo kwa kuvinufaisha viwanda 400 ambavyo hutumia malighafi za misitu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...