Na. Vero Ignatus, Arusha

Katibu Mkuu mtendaji wa Smaujata amewataka Viongozi kusimamia vyema nafasi walizonazo sambamba na kuwa barua njema kwa kila anayewasoma

Ameyasema hayo katika kikao cha Viongozi wa Smaujata mkoa kilichofanyika Jijini Arusha, ambapo aliwataka kutambua kuwa Uongozi ni majukumu poa ni mgumu,kwani hawawezi kupendwa na kila mtu badala yake kila mmoja wao atambue nafasi yake, waitumikie jamii kwa moyo wa huruma,kwa kusimamia haki, pamoja na kuwa na kifua cha kubeba mambo.

Aidha aliwataka Viongozi hao wajitahidi kuwa waadilifu kwenye nafasi zao, watafute namna wanaweza kutengeneza utaratibu wa kufuatilia mambo pamoja na kutoa nafasi kwa wengine, zaidi kufahamu mipaka yao ya kiutendaji.

"Ninyi kama Mashujaa na Viongozi ni vyema kutambua kwa kupitia uzoefu wa namna moja ama nyingine mnaweza kuangalia namna gani njema ya kutatua changamoto"alisema Injinia Juliana

Akisoma ripoti ya utendaji wa kazi katika mkoa Kaimu Katibu wa Smaijata
Lussa Melembuki alisema kuwa hadi sasa wameweza kufikia jumla ya shule za msingi zaidi ya 246,shule za sekondari zaidi ya 118,Makanisa 42, wamefanya semina 12 pamoja na kushiriki zaidi ya matamasha 18 vyote hivyo ni kwaajili ya outta elimu kwa jamii dhidi ya Ukatili

Vile vile ameweza kuushukuru Uongozi wa seriali ngazi ya mkoa kwa kuwapatia ushirikiano mkubwa kwani wamekuwa sababu ya wao kufanikisha kutoa elimu katika jamii, ikiwemo kuwajuza madhara yatokanayo na Ukatili, na mahali sahihi pa Kutoa taarifa endapo wataona dalili ama jambo lolote lenye viashiria vya ukatili.

Aidha ifahamike kuwa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii Tanzania ni kampeni mahususi ya Kitaifa kwaajili ya kupinga, kuibua na kutokomeza vitendo vyote vya ukatili katika Jamii zote nchini, kuelimisha Jamii kuondokana na fikra, Imani, Mila na desturi na tamaduni zinazokinzana na Maendeleo.

Baadhi ya malengo ya kampeni hiyo ni kutambua kutengeneza mtandao Jamii, sense uwezo wa kupaza Sauti kupinga nakupambanaa na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na Watoto, kuelimisha na kurahisisha utambuzi na ufanyiaji kazi viashiria vyote vya ukatili kuanzia ngazi ya Familia.






Katibu Mkuu wa Shujaa wa Maendeleo na Ustawi wa Jamii (Smaujata)nchini Mhandisi Juliana Marko akizungumza na Viongozi wa Wilaya pamoja na wale wa mkoa alipotembelea Jijini hapo kwaajili ya shughuli za kikazi kushoto kwake ni Mwenyekiti wa mkoa wa Arusha Godfrey Zablon.


Katibu Mkuu Smaujata Taifa wa pili kutoka kushoto Juliana Marko akiwa katika picha ya pamoja na Viongozi wa Mkoa wa Arusha mapema Marchi 27,2024

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...