Na WAF - Mwanza

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema dozi Moja ya chanjo ya HPV inatosha kumkinga msichana kupata ugonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi na kuwataka wazazi/walezi kuwapeleka watoto kupata chanjo hiyo.

Waziri Ummy amesema hayo leo Aprili 22, 2024 kwenye uzinduzi wa Maadhimisho ya Dozi moja ya chanjo ya HPV kwa wasichana wenye umri wa miaka 9 hadi 14 iliyozinguliwa katika viwanja vya Furahisha Wilayani Ilemela Mkoa wa Mwanza.

“Wataalamu wetu ambao wanatoka kwenye Taasisi ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR) wametuhakikishia kuwa dozi moja ya chanjo ya HPV inatosha kumkinga msichana kupata Saratani ya Mlango wa Kizazi”. Amesema Waziri Ummy

Amesema, awali dozi zilizokuwa zinatolewa mbili, ya kwanza inatolewa leo na baada ya miezi Sita inatolewa nyingine hii ilikua inapelekea mabinti wengi kutorudi kupata dozi ya pili, Sasa hivi tumeamua kutoa dozi moja ya HPV kwa kuwa inatosha kuwakinga wasichana kuja kupata maambukizi ya Saratani ya Mlango wa Kizazi.

Aidha, Waziri Ummy amesema Saratani inayoongoza kuwatesa Watanzania ni Saratani ya Mlango wa Kizazi ambapo amesema katika kila wagonjwa 100 wanaougua Saratani, wagonjwa 23 ni wagonjwa wa Saratani ya Mlango wa Kizazi.

“Inafuata Saratani ya mfumo wa chakula asilimia 11, Saratani ya Matiti asilimia 10.4, Saratani ya tezi dume asilimia 8.9 kwa hiyo ukiaangalia hapo Saratani inayoongoza ni Saratani ya Mlango wa Kizazi”. Amesema Waziri Ummy

Waziri Ummy ametoa wito kwa wazazi na walezi wote nchini, kuhakikisha watoto wanapata chanjo zote wanazopaswa kupata kwa kuwa lengo kubwa la chanjo ni kuwakinga na magonjwa yakiwemo haya ya Saratani pamoja na kuwakinga na vifo vinavyoweza kuzuilika na chanjo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana Mhe. Amina Makilagi akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa Mwanza Mhe. Saidi Mtanda amesema watahakikisha watoto wote wenye umri wa kuanzia miaka 9-14 wanapata chanjo hiyo ili kufikia malengo.

“Kwa mwaka 2022/23 Mkoa wa Mwanza ulifanikiwa kuchanja watoto zaidi ya laki Mbili sawa na asilimia 107 kati ya walengwa waliotarajiwa kuchanjwa ni laki 191,440 wenye umri chini ya Mwaka Mmoja, tumefikia malengo na kuyavuka”. Amesema Mhe. Makilagi








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...