NA WILLIUM PAUL, ROMBO.

MBUNGE wa Rombo ambaye ni Waziri wa Elimu Sayansi na teknolojia, Profesa Adolf Mkenda amesema mgawanyo wa fedha zinazotolewa na serikali katika tarafa mbalimbali ndani ya wilaya ya Rombo haufanywi kwa upendeleo bali kwa kuzingatia uhitaji katika kila eneo.

Pia amesema kwa kipindi Cha miaka 3 , serikali imetenga mamilioni ya fedha kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika wilayani hiyo ikilinganishwa na kipindi cha Miaka 10 iliyopita.

Profesa Mkenda alisema hayo wakati akifanya mkutano wa ndani na wajumbe wa mkutano mkuu wa wilaya CCM kutoka katika Tarafa ya Mengwe kuelezea maendeleo yaliyofanywa na serikali ya awamu ya sita wilayani Rombo kwa kipindi cha miaka mitatu chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Akizungumzia mgawanyo huo wa fedha zilizotolewa na serikali kupitia halmashauri kwa kipindi cha miaka 3 Profesa Mkenda amesema , Tarafa ya Mkuu ilipata kiasi Cha bilioni 3.8, Mengwe bilioni 3.558, Tarakea bilioni 2.3 , Useri bilioni 2.419 huku Mashati ikipata zaidi ya kiasi Cha shilingi milioni 903.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...