-Dk. Mpango, Kinana, Nchimbi, Majaliwa washiriki

Na Mwandishi Wetu Zanzibar

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi amewaongoza wananchi na viongozi mbalimbali wa Chama na Serikali katika dua maalumu ya kumuombea Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Hayati Sheikh Abeid Amani Karume.

Dua hiyo ambayo imehudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali, vyama vya siasa, dini pamoja wananchi imefanyika leo Jumapili Aprili 7, 2024, katika Ofisi Kuu za Chama Cha Mapinduzi (CCM), Kisiwandui, Zanzibar ikiwa ni sehemu ya maadhimisho ya kumbukumbu ya kifo cha Hayati Sheikh Karume aliyeuwawa Aprili 7, mwaka 1972.

Miongoni mwa viongozi waliohudhuria dua hiyo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Philip Mpango, Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Komredi Abdulrahman Kinana, Katibu Mkuu wa CCM, Balozi Dk. Emmanuel John Nchimbi, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar, Othman Masoud, Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla pamoja na viongozi wengine waandamizi.




















Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...