Mkoa wa Singida umezindua rasmi zoezi la utoaji wa chanjo wa Saratani la mlango wa uzazi kwa wasichana mwenye umri kati ya miaka Tisa hadi 14 ambapo Wasichana 178, 114 wanatarajiwa kupatiwa chanjo hiyo mkoani humo.

Akizindua zoezi la utoaji wa Chanjo hiyo katika Kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida, Mkuu wa mkoa wa Singida Halima Dendego (leo 22-Apr-2024 ) amewaagiza Maafisa Afya wahakikishe maeneo yote yaliyoandaliwa kutolewa huduma hiyo ya chanjo yanafanya hivyo kwa viwango vya juu ili kuwalinda watoto wa kike na saratani hiyo hatari.

Halima Dendego amesisitiza kuwa chanjo hiyo pia ni lazima iwafikie wanafunzi wanaosoma kwenye shule binafsi na watoto wa kike ambao wanaishi mitaani nao wapate fursa ya kupata chanjo hiyo ili kuwakinga na saratari na mlango wa uzazi.

“Tunapoenda kuwalinda watoto wa kike kwa kuwachanja chanjo hiyo maana yake tunawaepusha na madhara ugonjwa wa saratani ili wasije wakaambuzi wavulana”Ameeleza Halima Dendego.

Amesisitiza kuwa chanjo hiyo ni muhimu kwa wasichana na inatolewa bure kwa sababu Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa maendeleo imegharamia chanjo hiyo, hivyo ni muhimu kwa wazazi na walezi kuwapeleka watoto wao kupata chanjo hiyo ili kuwaepusha na madhara yanayoweza kutokea.

Naye, Mganga Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt Victorina Ludovick amesema kwa Tanzania chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi (HPV) ilianza majaribio mwaka 2014 mkoani Kilimanjaro na kupata mafanikio makubwa kwa kuwakinga wasichana wasipate ugonjwa huo.

Dkt Victorina Ludovick ameeleza mtu yeyote anaweza kuambukizwa saratani hiyo katika umri wowote ule hasa wakati wa tendo la ndoa na inaweza kusababisha magonjwa mengine ikiwemo saratani ya koo na magonjwa mengine ya via vya uzazi kwa wanamke na wanaume.

Kwa upande wake, Katibu Tawala wa mkoa wa Singida Dkt Fatuma Mganga amewataka Maafisa Afya wanatoa chanjo hiyo kuhakikisha wanafanikisha zoezi hilo kwa viwango ili mkoa wa Singida uwe wa kwanza katika utoaji wa chanjo hiyo kwa wasichana mwenye umri wa miaka Tisa hadi 14.

Amesema saratani hiyo inaua na ni ugonjwa hatari hivyo ni muhimu kwa watoto wote wenye umri wa kupata chanjo wapewe chanjo hiyo kutokana na umuhimu wake katika kulinda afya zao.

Nao, Mashuhuda waliopewa chanjo hiyo wakizungumza kwenye uzinduzi wa utoaji wa chanjo ya satarani la mlango wa uzazi katika kijiji cha Kisaki Manispaa ya Singida Lukuresia Andrea na Salisabila Athumani wote wakazi wa mkoa wa Singida wamesema tangu wapatiwe chanjo hiyo hawajapata madhara yeyote hivyo wameomba wazazi na walezi wasiwauzie watoto wao wa kike kwenda kupata chanjo hiyo kwa sababu inafaida kubwa katika maisha yao.
Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Victorina Ludovick akimchoma sindano ya chanjo mwanafunzi wa shule ya msingi Kisaki
 

 Mkuu wa Mkoa wa Singida Halima Dendego akizungumza kwenye uzinduzi wa zoezi la utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi
 

Mganga Mkuu wa Mkoa wa Singida Victorina Ludovick akisoma taarifa ya utoaji wa chanjo katika mkoa wa Singida
 

Wanafunzi kutoka Shule mbalimbali waliohudhuria zoezi la utoaji wa chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi katika kijiji cha kisaki.
 

Wanawake waliopata chanjo ya Saratani ya mlango wa kizazi Mkoani Singida wakiwa na watoto wao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...