NA WILLIUM PAUL, SAME.

MKUU wa Wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro Kasilda Mgeni ameeleza kusikitishwa na kitendo cha Wakala wa maji safi na usafi wa Mazingira vijijini (RUWASA) wilayani humo kushindwa kushirikisha jamii husika kwenye maeneo mbalimbali ambako kunatekelezwa miradi ya maji hali inayopelekea kutokea malalamiko kutokana na kutoelewa nini kinaendelea.

Kasilda ameeleza hayo baada ya malalamiko ya wakazi wa Kijiji cha Bangalala kwenye mkutano wa hadhara wakidai kusitishiwa huduma ya maji kwenye jumuiya ya watumia maji Mhetute takribani miezi mitatu pasipo kupatiwa taarifa yeyote kutoka kwa mamlaka husika.

"Waziri wa Maji Jumaa Aweso yupo vizuri sana lakini tukija huku chini mnamuangusha sana, yani lazima mbadilike RUWASA haiwezekani ulete mradi kwenye Kijiji halafu wananchi wa eneo husika hawajui chochote kuhusu huo mradi". Alisema Kasilda.

Aidha amemuagiza Afisa Tarafa ya Mwembe Mbaga, kuitisha mkutano wa hadhara ndani ya wiki moja kutekeleza takwa la kisheria kuchagua viongozi watakao simamia mradi huo kuwa na matumizi endelevu, ambapo pia husaidia kudhibiti kuhujumiwa kwa miradi inayotekelezwa kwani wananchi watakuwa na ufahamu juu ya utekelezaji wake.




Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...