Na Mwandishi Wetu

MKURUGENZI wa Msama Promotion, Alex Msama amewaomba Watanzania kukumbuka na kuenzi mambo mema yaliyofanywa na aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Mbunge wa Mtama hayati Benard Membe wakati wa uhai wake.

Pia amewaomba kuendelea kuyasimamia yale yote mema ambayo Membe enzi za uhai wake alikuwa anataka yatekelezwe.

Akizungumza katika Misa ya Kumkumbuka Hayati Benard Membe iliyofanyika Kanisa la St. Joseph jijini Dar es Salaam Msama amesema Hayati Membe ameacha alama ndani ya Serikali katika nafasi mbalimbali alizotumikia ikiwemo ya Waziri wa Mambo ya nje, kwani matunda na alama aliyoicha inaigusa nchi.

Amesema wakati kesho Membe anatimiza mwaka mmoja tangu afariki dunia,Msama amesema kuna mambo mengi amefanya katika Taifa letu na kuna mengine aliyoawaachia Watanzania ili wayaendeleze.

"Kikubwa ambacho Hayati Membe ametuachia sisi watu wake wa karibu, tuwe wamoja, tusameheahane tunapokoseana...tusiwe watu wa kuzungumziana mambo yasiyosahihi .Pia tuwe wazalendo katika Taifa letu la Tanzania ili tuweze kuwasaidia na wengine ambao wanatakiwa kuinuliwa,"amesema Msama.

Ameongeza Watanzania wasisahau kumcha Mungu,wajitolee katika kazi za Mungu."Tuwe  tunasaidia miradi ya kazi za Mungu kwa lengo la kufanikisha kazi za Mungu zinasonga mbele. Sisi watu wake wa karibu na Hayati Membe, tunaendelea kuyaenzi yale ambayo yanatakiwa kuyafanya”




Kwa upande wake Waziri wa Habari , Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema wamekuwa na siku nzuri ya kutafakari kazi nyingi alizozifanya Hayati Membe nchini, hasa katika jimbo la Mtama alikozaliwa.

Amefafanua kuwa katika kumuenzi Membe wameandaa Misa ya kumkumbuka na kumuombea kwa Mungu."Kesho kaka yetu Benard Membe anatamiza mwaka mmoja tangu alipofariki Dunia.Tumekuwa na siku nzuri ya kutafakari kazi nyingi alizozifanya katika nchi yetu, katika jimbo la Mtama."

Akieleza zaidi Waziri Nape amesema kuwa katika Jimbo la Mtama, Hayati Membe alikuwa ni muumini wa kubadilisha maisha ya watu kwani wakati wa uongozi wake alikuwa akitamani kila mtu awe na maisha mazuri.

Amefafanua Hayati Membe alitamani  mtu aishi kwenye nyumba nzuri, apate maji safi, na hizo ndizo ndoto ambazo ameendelea nazo."Ndio maana tangu aliponiacha tumehakikisha tumesambaza umeme katika Jimbo letu.

"Tumepeleka maji kila mahali, mawasiliano, shule, na katika Kijiji na Kata aliyotoka wakati anaondoka hakukuwa na sekondari, hivyo tumejenga sekondari na tukaipa jina lake Benard Membe ili kumkumbuka."



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...