Na Mwandishi wetu Mirerani

TAASISI ya Akhsante Foundation Tanzania imechinja ng'ombe 350, kondoo na mbuzi 1,800 za nyama na kugawa kwa yatima, wajane, wahitaji na taasisi mbalimbali za mji mdogo wa Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Eid El Adha.

Nyama hizo zimechinjwa kwa ajili ya kusherehekea sikukuu ya Eid El Adha mji mdogo wa Mirerani na kusimamia na taasisi ya kijamii ya Akhsante Foundation Tanzania ambayo inaendesha shughuli zake sehemu mbalimbali za Tanzania bara.

Mkurugenzi wa taasisi hiyo Katada Hashimu Kimaro amesema wamechinja ng'ombe 350 kondoo na mbuzi 1,800 na kugawa nyama hizo kwa wahitaji.

Kimaro amesema lengo ni kuhakikisha wahitaji wanapatiwa msaada huo ili waweze kusherehekea sikukuu ya Eid El Adha kwa furaha na amani.

"Tunatarajia kukamilisha shughuli hiii kwa muda wa siku mbili kwa kuhakikisha walengwa wote wanapata nyama hizo kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hii ya Idd," amesema Kimaro.

Amesema wajane, yatima, vituo vya watoto wenye uhitaji na taasisi mbalimbali za eneo hilo zimegawiwa nyama hizo kwa ajili ya kusherehekea sikukuu hiyo.

Mmoja kati ya wakazi wa mji mdogo wa Mirerani, Asia Juma amesema amesherehekea sikukuu hiyo kwa kupatiwa nyama ya mbuzi atakayotumia na watoto wake.

"Sisi wajane tumeshukuru kwa kupatiwa msaada huu ambao kwa namna moja au nyingine utatusaidia katika kusherehekea sikukuu hii," amesema.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...