Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imezindua ‘Akaunti ya Mfugaji’ mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini wakiwemo wafugaji, wanenepeshaji mifugo, wafanyabiashara wa mifugo, wasafirishaji wa mifugo mifugo na wadau mbalimbali wanaohudumia sekta hiyo muhimu kiuchumi.
Huduma
hiyo ya kwanza kutambulishwa na benki ya biashara nchini maalumu kwa
kundi hilo, pamoja na kuchochea kasi ya ukuaji wa sekta hiyo kupitia
huduma za fedha zilizorahisishwa zaidi pia inalenga kuunga mkono
jitihada za serikali katika kuandaa uchumi jumuishi kwa makundi yote ya
uzalishaji kupitia huduma bora za kifedha.
Hafla ya utambulisho
wa huduma hiyo kitaifa imefanyika leo kwenye soko la mnada wa mifugo la
Pugu lililopo wilayani Ilala, jijini Dar es Salaam, ikiongozwa na Mkuu
wa wilaya hiyo (DC), Edward Mpogolo sambamba na viongozi wengine
waandamizi wa wilaya hiyo, wadau wa biashara ya mifugo wakiwemo
viongozi na wafanyabiashara wa soko hilo. Mkurugenzi wa Idara ya wateja
wadogo na Wakubwa wa benki ya NBC Elibariki Masuke aliwaongoza maofisa
wengine wa benki hiyo kwenye uzinduzi huo.
Akizungumza kwenye
hafla hiyo, DC Mpogolo pamoja na kuipongeza benki ya NBC kwa kubuni
huduma hiyo muhimu, alisema ujio wa huduma hiyo ni ukombozi mkubwa kwa
wadau wa sekta ya mifugo nchini kutokana na uwepo wa changamoto ya
ukosefu wa huduma za kibenki zinazoendana na mahitaji maalum ya kundi
hilo hali ambayo imekuwa ikisababisha wengi wao kuamua kutumia huduma za
kifedha zisizo rasmi na hivyo kuhatarisha usalama wao na fedha zao.
“Kwa
mfano katika mnada huu wa Pugu unahusisha mzunguko wa fedha wastani wa
kiasi cha Tsh bilioni 1 kila siku huku wengi wa wafanyabiashara
wakilazimika kutembea na fedha taslimu kitu ambacho ni hatarishi kwao
binafsi na mitaji yao. Hivyo ujio wa huduma hii ya Akaunti ya Mfugaji
iliyobuniwa kwa ajili yao utakuwa suluhisho la changamoto hii kwasababu
huduma za kifedha ikiwemo miamala zitapatikana kwenye maeneo ya minada
hii karibu yao kabisa,’’ alisema.
Hata hivyo Mpogolo aliiomba
benki hiyo kupitia huduma hiyo kuhakikisha inawasaidia zaidi wafugaji
kwa kuwekeza zaidi kwenye suala zima la utoaji wa elimu ya fedha, elimu
kuhusu ufugaji wa kisasa na elimu ya masoko ili wafugaji wawaweze
kunufaika zaidi na idadi kubwa ya mifugo waliyonayo kupitia ufugaji na
uwekezaji wa kisasa kwenye sekta hiyo.
Awali akiizungumzia
huduma hiyo, Masuke alisema inahusisha wafugaji mmoja mmoja na vikundi
huku ikitoa faida mbalimbali kwa wafugaji hao ikiwemo mikopo mbalimbali
kwa waufugaji na biashara wa sekta hiyo huku ikiwa haiusishi makato ya
uendeshaji wa akaunti kila mwezi, kupata taarifa za akaunti bila makato,
gharama nafuu za utoaji wa fedha, huduma za kibenki kwa njia ya simu
(NBC Kiganjani) huku muhusika akinufaika na nyongeza ya asilimia 2
kwenye akiba yake kila mwezi.
“Kwa upande wa wafugaji wa vikundi
au vyama pia hawatakiwi kuwa na hofu sababu watakuwa na uhuru wa kuweka
na kutoa fedha zao wakati wowote na pia watapata kitabu cha hundi kwa
gharama nafuu wachotakiwa ni kufungua akaunti bure kabisa kwenye matawi
yeto kote nchini,’’. Alisema.
Akifafanua zaidi kuhusu huduma
hiyo Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo, Lariba na wakulima kutoka
Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa alisema inahusisha wafugaji wa mifugo
ya aina zote wakiwemo ng’ombe na kuku na hatua hiyo ni mwendelezo wa
jitihada za benki hiyo kuyafikia makundi yote ya uzalishaji kufuatia
uzinduzi wa huduma kadhaa za mahususi kwa wakulima ikiwemo bima ya afya.
“Ni karibuni tu tumetoka kuzindua huduma ya Bima kwa wakulima
nchini nzima sambamba na sasa ni wakati muafaka pia kuwageukia wafugaji
nao waweze kunufaika na huduma hizi za NBC mahususi kwao ikiwemo huduma
hiyo ya bima,’’ alisema.
Wakizungumzia huduma hiyo, Mkuu wa
Mnada wa Pugu, Noel Byamungu na Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mifugo
kwenye mnada huo, Iddy Maziku walisema imekuja wakati muafaka na itakuwa
suluhisho kwa wafugaji, wafanyabiashara wa mifugo na wadau wengine
sokoni hapo ambao kwasasa baadhi yao wanalazimika kutembea na kiasi
kikubwa cha fedha taslimu kwenye mifuko kutokana na kutokuwepo kwa
huduma za kifedha zinazoendana na mahitaji yao karibu na maeneo ya
minada hiyo.
“Ujio wa huduma hii utatusaidia kwa kiasi kikubwa
sisi wadau wa sekta hii ya mifugo. Inawezekana tayari tunahudumiwa na
taasisi za nyingine za kifedha zikiwemo zile ambazo sio rasmi lakini
ujio wa huduma hii mahususi kwa ajili yetu itakuwa ni suluhisho na
kambilio kwetu. Tunaamini kupitia huduma hii sasa hatulazimika tena
kutembea fedha taslimu ili kufanya malipo ya manunuzi ya mifugo na
huduma nyingine. Uzuri zaidi huduma hizi sasa zitakuwa zinatufuata
mahali tulipo na hivyo kutuhakikishia usalama wetu na fedha zetu…kwa
hili tunawashukuru sana NBC,’’ alisema Maziku.
Mkuu wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo (wa nne kulia)maoifisa wa benki ya NBC akiwemo sambamba na wadau wengine wa sekta ya mifugo wakiwemo Mkurugenzi wa Idara ya wateja wadogo na Wakubwa wa benki ya NBC Elibariki Masuke (wa tatu), Mkuu wa Idara ya Masoko ya benki hiyo David Raymond (wa sita kulia) pamoja na wadau wa biashara ya mifugo wakimsiliza Mkuu wa Mnada wa mifugo kwenye soko la mifugo la Pugu, Noel Byamungu akielezea kuhusu hali ya biashara kwenye mnada huo wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa ‘Akaunti ya Mfugaji’ ya benki ya NBC mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada huo.
Mkuu wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo (alievaa suti) sambamba na maoifisa wa benki ya NBC akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya wateja wadogo na Wakubwa wa benki ya NBC Elibariki Masuke (katikati alievaa kofia) sambamba na wadau mbalimbali wa sekta ya mifugo wakiwemo wafanyabishara wa mifugo wakionyesha huduma mbalimbali zinazopatikana kupitia ‘Akaunti ya Mfugaji’ ya benki ya NBC wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa akaunti hiyo mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam.
Akizungumza kwenye hafla hiyo, DC Mpogolo pamoja na kuipongeza benki ya NBC kwa kubuni huduma hiyo muhimu, alisema ujio wa huduma hiyo ni ukombozi mkubwa kwa wadau wa sekta ya mifugo nchini kutokana na uwepo wa changamoto ya ukosefu wa huduma za kibenki zinazoendana na mahitaji maalum ya kundi hilo hali ambayo imekuwa ikisababisha wengi wao kuamua kutumia huduma za kifedha zisizo rasmi na hivyo kuhatarisha usalama wao na fedha zao.
Awali akiizungumzia huduma hiyo, Masuke (pichani) alisema inahusisha wafugaji mmoja mmoja na vikundi huku ikitoa faida mbalimbali kwa wafugaji hao ikiwemo mikopo mbalimbali kwa waufugaji na biashara wa sekta hiyo huku ikiwa haiusishi makato ya uendeshaji wa akaunti kila mwezi, kupata taarifa za akaunti bila makato, gharama nafuu za utoaji wa fedha, huduma za kibenki kwa njia ya simu (NBC Kiganjani) huku muhusika akinufaika na nyongeza ya asilimia 2 kwenye akiba yake kila mwezi.
Akifafanua zaidi kuhusu huduma hiyo Mkuu wa kitengo cha wateja wadogo wadogo, Lariba na wakulima kutoka Benki ya NBC, Bw Raymond Urassa (pichani) alisema inahusisha wafugaji wa mifugo ya aina zote wakiwemo ng’ombe na kuku na hatua hiyo ni mwendelezo wa jitihada za benki hiyo kuyafikia makundi yote ya uzalishaji kufuatia uzinduzi wa huduma kadhaa za mahususi kwa wakulima ikiwemo bima ya afya.
Akizungumzia huduma hiyo, Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mifugo kwenye mnada huo, Iddy Maziku (Pichani) alisema imekuja wakati muafaka na itakuwa suluhisho kwa wafugaji, wafanyabiashara wa mifugo na wadau wengine sokoni hapo ambao kwasasa baadhi yao wanalazimika kutembea na kiasi kikubwa cha fedha taslimu kwenye mifuko kutokana na kutokuwepo kwa huduma za kifedha zinazoendana na mahitaji yao karibu na maeneo ya minada hiyo.
Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa mifugo kwenye mnada wa Pugu, Iddy Maziku (kushoto) akifungua akaunti ya mfugaji ya benki ya NBC wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa akaunti hiyo mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam.
Baadhi ya wadau wa sekta ya mifugo wakiwemo wafanyabishara wa mifugo wakifuatilia uzinduzi wa akaunti ya mfugajiya benki ya NBC wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa akaunti hiyo mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam
Mkuu wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo (alievaa suti) akimpongeza Mkurugenzi wa Idara ya wateja wadogo na Wakubwa wa benki ya NBC Elibariki Masuke kwa ujio wa ‘Akaunti ya Mfugaji’ ya benki ya NBC mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Idara ya Masoko wa benki ya NBC David Raymond akionyesha huduma mbalimbali zinazopatikana kupitia ‘Akaunti ya Mfugaji’ ya benki ya NBC wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa akaunti hiyo mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo (alievaa suti) sambamba na maoifisa wa benki ya NBC akiwemo Mkurugenzi wa Idara ya wateja wadogo na Wakubwa wa benki ya NBC Elibariki Masuke (katikati alievaa kofia) sambamba na wadau mbalimbali wa sekta ya mifugo wakiwemo wafanyabishara wa mifugo wakionyesha huduma mbalimbali zinazopatikana kupitia ‘Akaunti ya Mfugaji’ ya benki ya NBC wakati wa hafla fupi ya uzinduzi wa akaunti hiyo mahususi kwa ajili ya wadau wa sekta ya ufugaji nchini. Uzinduzi huo ulifanyika mwishoni mwa wiki kwenye mnada wa mifugo wa Pugu jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...