Wanahisa wa Benki ya NMB wameidhinisha gawio la Shilingi Bilioni 181, sawa na shilingi 361 kwa kila hisa moja kwa mwaka unaoishia Disemba 31, 2023.

Azimio hilo limepitishwa leo wakati wa Mkutano Mkuu wa 24 wa Wanahisa wa Benki ya NMB.

Hili ni ongezeko la 26% ukilinganisha na gawio la jumla la Shilingi Bilioni 143.1 tulilolipa mwaka 2022, na kuandika historia mpya ya kuwa gawio kubwa zaidi kuwahi kutolewa na taasisi ya fedha nchini kwa wanahisa wake.

Mafanikio haya ni matokeo ya mazingira mazuri ya kibiashara yaliyowekwa na Serikali yetu, imani ya wanahisa na wateja wetu, juhudi za wafanyakazi wetu na ushirikiano mzuri tulionao na wadau wetu wote.

Tutaendelea kusimamia ahadi yetu ya kudumu katika ukuaji jumuishi na endelevu kwa ustawi wa jamii tunayoihudumia na uchumi wa nchi yetu ya Tanzania kwa ujumla.

Tunawashukuru wadau wetu wote kwa kuwa sehemu ya mafanikio haya.

#NMBAGM2024 #NMBKaribuYako








Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...