Silas Matoi (katikati), Mkuu wa Idara ya Njia Mbadala za Kidijitali wa Exim Bank, akitangaza washindi 10 wa droo ya kwanza ya kampeni ya Tap Tap Utoboe yenye lengo la kuwahamasisha wateja wa benki hiyo kufanya miamala yao kutumia simu za mkononi na mtandao kufanya miamala ya malipo.
Kampeni hii ya miezi mitatu inatoa washindi wa kila wiki na mwezi ambao wanajishindia fedha taslimu na mwishoni kutakuwa na washindi wa pikipiki, bajaji na mshindi wa kwanza atajinyakulia gari mpya.
Kushoto ni Mkaguzi na Mdhibiti wa michezo ya kubahatisha kutoka Bodi ya Michezo ya Kubahatisha Tanzania, Salim Bugufi na Thuweiba Bakary, Afisa wa benki hiyo wakiwa katika droo hiyo iliyofanyika tarehe 19 Juni, 2024 katika Makao Makuu ya Exim Bank jijini Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...