Staa wa muziki kutoka Nigeria, Akumefule Chukwuemeka Georg maarufu kama Blaqbonez anayewakilisha lebo ya Chocolate City Music, Julai 19,20024 leo anatarajia kuachia kazi yake mpya iitwayo Fire On Me”.
Mkali huyo anaachia kazi yake hiyo huku akiwa amepata mafanikio makubwa kupitia albamu yake ya tatu iitwayo “Emeka Must Shine”.
Kwenye ngoma yake hii mpya ya "Fire on Me” anapita vizuri kwenye misingi ya Hip Hop katika kila mstari, na unavuta hisia na kukonga moyo.
"Sex Over Love" ndio Albamu ya kwanza ya
Blaqbonez ambayo ilitoka 2021, na ilishika nafasi ya kwanza kwa kuwa Albamu ya #1 nchini Nigeria kwenye Apple kwa wiki tatu mfululizo; Wimbo #1 nchini Nigeria - Apple kwa wiki moja; #2 Nyimbo 100 Bora - Deezer.
Mwaka 2022 aliachia albamu ya “Young Preacher” na 2013 albamu ya “Emeka Must Shine” ilitoka.
Kazi za msanii huyu zimetajwa kuwavutia mastaa wakubwa kama
Amaarae, Ludacris, Zlatan, ODUMODUBLVCK. Lojay, Blxckie, na wengine na kitajwa kama wasanii wa kuvutia wa hip hop barani Afrika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...