NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

TIMU ya Taifa ya Hispania imefanikiwa kunyakua kombe la Euro 2024 mara baada ya kuichapa Uingereza mabao 2-1 katika fainali ambayo imepigwa kwenye dimba la Olympiastadion (Berlin) nchini Ujerumani.

Hispania walianza kupata bao kupitia kwa Nico Williams dakika ya 47 kipindi cha pili akipokea pasi kutoka kwa nyota Yamal.

Dakika ya 72, nyota anaekipiga kwenye klabu ya Chelsea Cole Palmer aliweza kuisawazishia timu yake kwa bao zuri akipokea pasi kutoka Jude Belligham.

Mikel Oyarzabal aliweza kufunga hesabu kwenye fainali hiyo kwa kupachika bao la pili na la ushindi akipokea pasi kutoka kwa Marc Cucurella dakika ya 86 ya mchezo.

Mchezaji bora wa mashindano tuzo imekwenda kwa nyota wa Machester City, Rodri.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...