KAMISHNA Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Yusuph Mwenda amekutana na kuzungumza na wafanyabiashara mkoani Dodoma.
Akizungumza na wafanyabiashara hao Julai 24 mwaka huu, Kamishna Mwenda ameahidi kufanya kazi kwa ukaribu na wafanyabiashara hao pamoja na kutatua changamoto zao za kikodi kwa wakati ili kuleta ari ya ulipaji kodi wa hiari.
Wafanyabiashara hao wamemshukuru na kumpongeza Kamishna Mkuu huyo kwa kutenga muda wake na kuwasikiliza na kujenga ari ya kulipa kodi kwa hiari.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...