Na Mwandishi wetu - Dodoma

Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia masuala ya Sera Bunge na Uratibu Mhe. Ummy Nderiananga leo tarehe 10 Julai, 2024 amekagua maandalizi ya Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa inayotarajiwa kufanyika tarehe 25 Julai, 2024 jijini Dodoma.

Mhe. Ummy ameridhishwa na maandalizi hayo yanayoendelea na anaimani kwamba maandalizi hayo yatazidi kufanyika vizuri na yatakamilikalika kwa wakati.

Aidha, maadhimisho hayo yatashirikisha gwaride la Majeshi ya Ulinzi na Usalama lenye vikosi vitano ambavyo ni Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Jeshi la Kujenga Taifa (JKT), Jeshi la Poliosi, Jeshi la Magereza pamoja na jeshi la Uhamiaji.

Awali akitoa maelezo kuhusu maandalizi hayo, Mkurugenzi wa Kitengo cha Maadhimisho na Sherehe za Taifa Ofisi ya Waziri Mkuu Bw. Batholomeo Jungu amebainisha kuwa, maadhimisho hayo yatatanguliwa na uwashaji wa Mwenge siku ya tarehe 24 Julai, 2024 usiku ambapo Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Dodoma.

Maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa yatafanyika tarehe 25 Julai, 2024 jijini Dodoma ambapo Mgeni Rasmi wa Maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mheshimiwa. Samia Suluhu Hassan.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...