Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kulifungua Tamasha la Mwaka Kogwa Makunduchi lililofanyika katika viwanja vya Kae Kuu Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja leo 16-7-2024 na (kulia kwa Rais) Mwenyekiti wa Kamati ya Mwaka Kogwa.Mwita Masemo Makungu na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Ayoub Mohammed Mahmoud.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akipata maelezo ya vyakula vya asili kutoka kwa Mzee wa Makunduchi Bi.Amina Ubwa Ali,baada ya kulifungua Tamasha la Mwaka Kogwa 2024, linalofanyika katika viwanja vya Kae Kuu Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja leo 16-7-2024.na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe.Ayoub Mohammed Mahmoud.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Wazee wa Kamati ya Mwaka Kongwa, alipowasili Makunduchi Mkoa wa Kusini Unguja kwa ajili ya ufunguzi wa Tamasha la Mwaka Kogwa lililofanyika leo 16-7-2024,katika viwanja vya Kae Kuu Makunduchi Wilaya ya Kusini Unguja.
(Picha na Ikulu)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...