NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

CHUO Kikuu Cha Dar Es Salaam, Ndaki ya TEHAMA wamebuni mfumo joto unaojiendesha kwa kujiongeza na kujipunguza joto kulingana na uhitaji wa wakati husika kwenye uhifadhi vyakula pamoja na kufuga kuku wa kisasa (broila).

Akizungumza leo Julai 5,2024 kwenye Maonesho ya 48 ya Biashara Kimataifa Sabasaba Jijini Dar es salaam Mhandisi wa Maabara, Ndaki ya Tehama Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Adriano Kamoye amesema kuku wa kisasa (broila) katika ukuaji wake wanahitaji joto kulingana na ukuaji wake.

"Katika ukuaji wa kuku wa kisasa, joto ni kitu cha muhimu sana, wafugaji wengi hutumia taa pamoja na mkaa, njia ambayo si salama katka ukuaji wa kuku hao, ndo maana tukaamua kuja na mfumo huu wa kisasa ambao ni bora na ni salama kwenye ufugaji" amesema

Aidha amesema kuwa Mfumo huo pia unaweza kutumika katika kuhifadhi mazao wakati wa usafirishaji na utunzaji kwa lengo la kuhifadhi ubora wa matunda au mbogamboga.

"Mbogamboga zinahitaji unyevunyevu wa kiasi fulani ili kuhifadhi ubora wake kwa muda mrefu, kwahiyo unyevunyevu ukiwa mkubwa au mdogo unaweza poteza ubora wake, kwahiyo mfumo huu unaweza kutuma katika mazingira hayo kutunza ubora wa matunda au mbogamboga"amesema.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...