NA EMMANUEL MBATILO, MICHUZI TV

CHUO Kikuu Cha Dar es Salaam, kupitia Mradi wa Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET), kimezindua Kamati ambazo zinafanya kazi kwenye maeneo ambayo wanafanya ujenzi ili kuwafikia wadau mbalimbali ambao watatoa maoni ambayo yatasaidia uboreshaji wa mradi wa (HEET).

Akizungumza na wandishi wa habari leo Julai 1,2024 katika Ukumbi wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam, Mtaalamu wa Masuala ya Usalama wa Mradi Dkt. Edmund Mabuye amesema wametoa mafunzo maalumu kwa kamati hizo sambamba na kuzirasimisha ili zianze kazi rasmi.

Aidha Dkt. Mabuye amesema kamati hizo zinafanya kazi kwa kuhusianisha vipengele mbalimbali ambavyo vinavyohusu usalama wa mradi kwa lengo la kuulinda.

"Maoni yanaweza kutolewa kwenye masuala yanayohusu jamii,yanayohusu Jinsia au yanayohusu masuala ya mazingira ambapo ni kamati moja inafanya kazi kwa kuzingatia vipengele mbalimbali vinavyohusu usalama wa mradi"Dkt.Mabuye amesema.

Kwa upande wake,Mkurugenzi wa Taasisi ya Taaaluma za Jinsia,Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Dkt. Lulu Mahaya amesema katika eneo la mahitaji maalumu kuna kipengele cha "Kaseme"ambacho kimejikita katika kupambana na unyanyasaji wa kijinsia hasa wa kingono.

Pamoja na hayo ameeleza kuwa lengo lao hasa ni kuzuia malalamiko kuwa kesi ambapo wamelenga kusimamia haki ili kuulinda mradi huo usisimamishwe kutokana na kufanyiwa ukatili kwenye maeneo ya ujenzi.

Mradi wa HEET unatarajiwa kufanyika kwa miaka mitano kupitia ufadhiri wa Benki ya Dunia,ambapo umekusudia kukuza elimu ya juu kama chachu ya uchumi mpya wa Tanzania,na kufufua na kupanua uwezo wa vyuo vikuu kuchangia katika maeneo muhimu ya uvumbuzi, maendeleo ya kiuchumi, na umuhimu wa soko la ajira.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...