Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kaimu Katibu Mkuu Kiongozi Bw. Mululi Majula Mahendeka, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemteua na kumuapisha Bw. Suleiman Abubakar Mombo kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa.
Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mombo alikuwa Afisa Mwandamizi wa Ofisi ya Rais, Ikulu. Bw. Mombo amechukua nafasi ya Balozi Ali Idi Siwa ambaye amestaafu.
Sharifa B. Nyanga
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...