Katika kesi ya mwandishi wa habari Eric Kabendera kwenye Mahakama Kuu ya Tanzania, ambapo amedai fidia ya dola milioni 10 dhidi ya Vodacom, kampuni hiyo imekanusha vikali madai hayo yaliyotolewa na Kabendera.
Akizungumza na vyombo vya habari, Mtaalamu Mwandamizi wa Sheria kutoka Vodacom, Joseph Tungaraza alisema, "Tunakanusha vikali madai ya mlalamikaji. Tunatoa huduma zetu kwa wateja wetu wote kwa kuchukua hatua madhubuti za faragha ya data. Kulinda usiri na usalama wa data zote ni jambo muhimu, na tunaendelea kutekeleza taratibu zote za kisheria za kulinda taarifa nyeti za wateja ila kuhakikisha uaminifu na faragha ya wadau wetu kwa ujumla unabakia kuwa kipaumbele chetu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...