WAZIRI wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) amefanya ziara ya ukaguzi katika maghala ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) yaliyopo eneo la Mazwi, Sumbawanga mjini, mkoani Rukwa tarehe 16 Julai 2024. 

Katika ziara hiyo, Bw. Marwa Range, Meneja wa Kanda ya Sumbawanga - NFRA alieleza kuwa uwezo wa kuhifadhi nafaka za mahindi katika eneo la Mazwi ni tani 28,500 ambapo zoezi la ununuzi linaendelea katika maghala hayo. 

Waziri Bashe alipata wasaha wa kukagua mizani ya digitali ambayo imeanza kutumika na kujiridhisha na shughuli ya upimaji wa nafaka unaondelea.  Aidha, alielekeza mizani iongezwe ili kuharakisha zoezi la upimaji kama sehemu ya utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan mapema leo wakati wa uzinduzi wa maghala ya NFRA katika eneo la Kanondo. 

Aidha, Waziri Bashe amefurahishwa kuona Wakulima mbalimbali wakiwasilisha mazao yao kwa maghala ya Mazwi na kusisitiza kasi ya upimaji iongezwe.  Vile vile, amemuelekeza Dkt. Andrew Komba, Afisa Mtendaji Mkuu wa NFRA kukarabati maghala hayo ili huduma kwa Wakulima zisikwame.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...