
Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan akizungumza kwenye Banda la NHIF wakati alipotembelea Maonesho Kitaifa Nane Nane yanayoendelea katika Viwanja vya Nzuguni jijini Dodoma.
Na Mwandishi Wetu,
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameutaka Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF), kuhakikisha wanawafikia wananchi wote ili wawe ndani ya mfumo wa Bima ya afya.
"Nataka bima kwa watu wangu wote, nitawaita tuzungumze" alisema Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Ameyasema hayo leo wakati akitembelea maonesho ya Nane Nane kitaifa mkoani Dodoma.
Hivi karibuni Mhe. Rais akiwa ziarani mkoani Katavi na Rukwa kwa nyakati tofauti alihamasisha wananchi kukata Bima ya afya ili wawe na uhakika wa kupata huduma za matibabu wakati wote.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...