
Wafanyakazi wa Barrick wakifurahi baada ya kumaliza kushiriki mbio hizo


Wafanyakazi wa Barrick wakishiriki kukimbia mbio za CRDB Bank Marathon 2024




Wafanyakazi wa Barrick wakishiriki kukimbia mbio za CRDB Bank Marathon 2024
Na Mwandishi Wetu.
Wafanyakazi wa kampuni ya Barrick nchini kupitia klabu zao za mchezo wa marathon wameshiriki katika mbio za msimu wa tano wa mbio za CRDB Bank Marathon, zilizofanyika jijini Dar es salaam.
Mbio hizo zililenga kuchangisha fedha kwa ajili ya kuchangisha fedha kwa ajili ya kusaidia watoto,huduma za afya kwa akina mama na vijana.
Wakimbiaji kutoka Barrick Runners clubs wamekuwa wakishiriki marathon mbalimbali zinazofanyika nchini na nje ya nchi hususani zinazolenga kuchangia kupambana na changamoto mbalimbali za kijamii.
Kampuni pia imekuwa na program za mazoezi kwa ajili ya wafanyakazi wake kwa ajili ya kuhakikisha wanakuwa na nguvu na afya bora pia imewekeza katika miundombinu ya michezo na mazoezi kwa ajili ya kuwawezesha wafanyakazi wake kushiriki michezo na mazoezi katika mazingira rafiki.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...