
Dkt. Tulia ameyasema hayo wakati akichangia kwenye Mkutano Mkuu wa 79 wa Umoja wa Mataifa (UNGA79) uliofanyika New York nchini Marekani leo tarehe 22 Septemba, 2024. Katika mchango wake amesisitiza kuwa juhudi za kusaidia nchi zinazoendelea kukuza uchumi zinapaswa kuongozwa na mikakati ya kimkakati, hususan katika kugawanya upya rasilimali za kiuchumi.
Dkt. Tulia amebainisha kuwa rasilimali nyingi ziko mikononi mwa wachache kitaifa na kimataifa jambo linalochangia kutokuwepo kwa usawa wa kiuchumi. Hivyo, amehimiza kuwa ipo haja ya kuweka mkazo mkubwa zaidi katika kuhakikisha ugawaji bora wa rasilimali hizo ili kufikia maendeleo endelevu na kupunguza pengo la kiuchumi kati ya mataifa na ndani ya mataifa husika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...