Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mashirika ya Umoja wa Mataifa jijini Vienna, Austria Mhe. Naimi Aziz amewasilisha Hati za Utambulisho kwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nguvu za Atomiki Duniani (IAEA) Mhe. Rafael Mariano Grossi katika tukio lililofanyika tarehe 10 Oktoba, 2024.

Wakizungumza baada ya tukio la kukabidhi Hati, viongozi hao wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na IAEA kwenye matumizi salama ya teknolojia ya nyuklia kwa ajili ya maendeleo ya sekta mbalimbali nchini hususan afya, kilimo na usalama wa chakula, afya, ufugaji na nishati.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...