Na Mwamvua Mwinyi, Chalinze Septemba 9, 2024
.jpeg)
.jpeg)
Amemtaka Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi na TBA wafike Chalinze kujionea na kujifunza katika ujenzi wa nyumba zao za kisasa ili kupata mbinu bora za kuboresha na kupunguza gharama za ujenzi wa nyumba hizo.
Aidha, Waziri Bashungwa amewataka watumishi kuwa wazalendo na kuacha urasimu wanapotoa huduma kwa wananchi .
Katika ziara hiyo, Waziri Bashungwa amezindua soko jipya la Chalinze lililogharimu sh. bilioni 1.7 na kuwashauri wajasiriamali kuwa wabunifu katika kuanzisha biashara tofauti ili waweze kupata soko kirahisi.
Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Miundombinu cha Halmashauri ya Chalinze, Injinia Olais Sikoi, ujenzi wa nyumba nane za wakuu wa idara ulianza mwaka 2022 na kufikia asilimia 98 kukamilika.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...