Shirika la Uwakala wa Meli Tanzania (TASAC) limeshiriki Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Lojistiki na Uchukuzi unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es salaam leo tarehe 17 Oktoba, 2024.

Mkutano huo umefunguliwa rasmi na Waziri wa Uchukuzi, Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb), ambaye katika hotuba yake ya ufunguzi amesema Serikali inatarajia kutumia kiasi cha Shilingi za Kitanzania bilioni 600 kwa ajili ya kugharamia miradi mitatu itakayoboresha huduma ya usafirishaji kwa njia ya maji mkoani Kigoma na maeneo yanayozunguka.

Mhe. Prof. Mbarawa amesema miradi hiyo ni pamoja na ujenzi wa kiwanda cha meli, ujenzi wa meli ya mizigo pamoja na meli ya kisasa ya abiria inayotarajiwa kufanya safari zake katika Ziwa Tanganyika na Ziwa Victoria.

“Bandari ya Kigoma ni muhimu kwa sababu kwenye Ziwa Tanganyika tunapakana na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kule kuna madini, kutokana na hilo kama Serikali tumeona tuweke
 

Mkurugenzi Mkuu wa TASAC Salum Mohamed akizungumza katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Lojistiki na Uchukuzi unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es salaam leo tarehe 17 Oktoba, 2024
Mkurugenzi  Mkuu wa TASAC  Salum Mohemed watatu kutoka kushoto akiwa katika Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Lojistiki na Uchukuzi unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es salaam leo tarehe 17 Oktoba, 2024
 

Waziri wa Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi  Mkuu wa TASAC Salum Mohamed wakati alipotembelea banda la TASAC katika maonesho kwenye  Mkutano wa Pili wa Kimataifa wa Lojistiki na Uchukuzi unaofanyika kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City Jijini Dar es salaam leo tarehe 17 Oktoba, 2024

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...