Vijana askari 80 wa Jeshi la Akiba (Mgambo) wamehitimu mafunzo yao ya miezi minne yaliyofanyika katika kata ya Bombo, Tarafa ya Gonja Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro, askari hao wamekula kiapo cha utii kwa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,tayari kufanya kazi kwa kujitolea kulitumikia Taifa kama walinzi wa usalama wa raia na mali zao.
Akihitimisha mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Same Kasilda Mgeni amawataka kutumia mbinu walizofundishwa kwa manufaa ya jamii, hususani kulinda raia na mali zao, kuzingatia matumizi sahihi ya Silaha Pamoja na mbinu mbalimbali walizojifunza na kuepuka kujihusisha na matukio ya uhalifu.
Aidha amewasisitiza askari hao kwamba Pamoja na wajibu wao wa msingi kwnye masuala ya usalama, askari hao ni kiungo muhimu kuhamasisha uzalendo kwenye jamii, kuunganisha Serikali na jamii hasa panapohitajika ushiriki wa raia katika shughuli za kijamii za kujitolea Pamoja na kuchangia miradi ya maendeleo hasa nguvu kazi.




Akihitimisha mafunzo hayo Mkuu wa Wilaya ya Same Kasilda Mgeni amawataka kutumia mbinu walizofundishwa kwa manufaa ya jamii, hususani kulinda raia na mali zao, kuzingatia matumizi sahihi ya Silaha Pamoja na mbinu mbalimbali walizojifunza na kuepuka kujihusisha na matukio ya uhalifu.
Aidha amewasisitiza askari hao kwamba Pamoja na wajibu wao wa msingi kwnye masuala ya usalama, askari hao ni kiungo muhimu kuhamasisha uzalendo kwenye jamii, kuunganisha Serikali na jamii hasa panapohitajika ushiriki wa raia katika shughuli za kijamii za kujitolea Pamoja na kuchangia miradi ya maendeleo hasa nguvu kazi.




Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...