Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo mkoa wa Iringa MWL Joseph Ryata amewaomba watanzania kujitokeza kujiandikisha kwenye zoezi la kupata vitambulisho vya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani 2025.

Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo mkoa wa Iringa MWL Joseph Ryata amewaomba watanzania kujitokeza kujiandikisha kwenye zoezi la kupata vitambulisho vya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani 2025.

Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo mkoa wa Iringa MWL Joseph Ryata akipokea cheti cha shukurani baada ya mafunzo ya walimu Makada wa CCM mkoani Songwe



Na Fredy Mgunda, Songwe.

Katibu wa itikadi, uenezi na mafunzo mkoa wa Iringa MWL Joseph Ryata amewaomba watanzania kujitokeza kujiandikisha kwenye zoezi la kupata vitambulisho vya mpiga kura kwa ajili ya uchaguzi mkuu mwakani 2025.

Akizungumza wakati wa mafunzo ya walimu Makada wa CCM mkoani Songwe, Ryata alisema kuwa moja ya jukumu kubwa la walimu ni kuhakikisha wanatoa elimu kwa wananchi wajitokeze kujiandikisha kwenye vitambulisho vya mpiga kura.

Ryata alisema kuwa kila mwananchi anahaki ya kuhakikisha anajitokeza kupata kitambulisho cha mpiga kura ili katika uchaguzi ujao aweze kuchagua viongozi anaowataka kuwaongoza kwa kipindi cha miaka mitano ijayo.

Alisema kuwa mwananchi asipokuwa na kitambulisho cha mpiga kura hatakuwa na haki ya kupiga kura kwa kiongozi yoyote katika uchaguzi mkuu mwakani 2025.

Nao baadhi ya walimu Makada wa CCM mkoa Songwe walisema kuwa wap tayari kuhakikisha wanatoa elimu kwa kila mwananchi kujitokeza kushiriki zoezi la kupata kitambulisho cha mpiga kura .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...