Na John Mapepele
Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi amesema Serikali kwa mara ya kwanza katika historia Desemba 20, mwaka huu inakwenda kuzindua tuzo za sekta ya Utalii na Uhifadhi.
Akuzungumza kwenye mkutano wa waandishi wa habari, Dkt. Abbasi amesema Wizara imeamua kufanya hiyo ili kutoa hamasa kwa wadau wa sekta hizo waweze kufanya vizuri hivyo kuchangia kwenye uchumi wa taifa.
Amefafanua kuwa ujumla ya tuzo 11 za heshima zitatolewa kwa wadau mbalimbali kutambua mchango wao katika sekta hizo.
Aidha, ameongeza kuwaTanzania imeendelea kufanya vizuri katika kupokea watalii wa kimataifa na kuvunja rekodi zilizowekwa kabla ya kipindi cha UVIKO – 19 mwaka 2019.
"Kwa mujibu wa Ripoti ya Nusu Mwaka ya Takwimu za Utalii ya Shirika la Utalii Duniani (UN Tourism Barometer report) katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Julai, 2024, Tanzania imeshika nafasi ya kwanza Afrika kwa nchi zilizotembelewa na idadi kubwa ya watalii." Amefafanua Dkt. Abbasi
Aidha, amesema tukio la uzinduzi wa tuzo hizo utaambatana na burudani mbalimbali za wasanii.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...