Mkutano wa Mawaziri wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) umefanyika Zanzibar tarehe 04 Januari, 2025 chini ya uenyekiti wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thatib Kombo akishirikiana na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Stergomena Tax.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Zambia na Malawi ambao ni wajumbe wa Utatu wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama (Organ Troika).

Mkutano huo ni maalum kwa ajili ya Maandalizi ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi hiyo utakaofanyika kwa njia ya mtandao tarehe 05 Januari, 2024.

Mkutano huo ulitoa mapendekezo ya namna SADC inavyoweza kuisaidia Jamhuri ya Msumbiji kukabiliana na changamoto za kisiasa zinazoendelea nchini humo, ambapo mapendekezo hayo yanatarajiwa kupitishwa na Wakuu wa Nchi na Serikali wa Organ Troika utakaongozwa na Mwenyekiti wake Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Msumbiji imekumbwa na machafuko ya kisiasa kufuatia chama cha upinzani kutokubaliana na matokeo ya uchaguzi mkuu wa nchi hiyo uliofanyika tarehe 09 Oktoba, 2024.














Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...