*Yapata kiasi cha Sh.bilioni 63.27 ikilinganishwa na Sh.bilioni 30 zilizopangwa kupatikana
Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA
 ya Masoko ya Mitaji na Dhamana(CMSA) imesema kuwa mauzo ya hatifungani 
ya benki ya Azania yamepata mafanikio ya asilimia 210.9,ambapo kiasi cha
 shilingi bilioni 63.27 kimepatikana ikilinganishwa na shilingi bilioni 
30 zilizopangwa kupatikana.
Aidha, asilimia 70 ya mauzo ya 
hatifungani imetoka kwa wawekezaji mmoja mmoja yaani Retail Investors na
 asilimia 30 imetoka kwa Kampuni na Taasisi. Kati ya wawekezaji wote 
walioshiriki, asilimia 98.4 ni wawekezaji wa ndani na asilimia 1.6 ni 
wawekezaji wa kigeni.
Hayo yamesemwa leo Januari 24,mwaka 2025 na
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana(CMSA), 
CPA. Nicodemus Mkama wakati wa hafla ya kuorodheshwa kwa toleo la kwanza
 la hatifungani ya Benki ya Azania(Azania Bond Yangu) katika Soko la 
Hisa la Dar es Saaam.
“Leo sekta ya masoko ya mitaji ina furaha 
kubwa kwa kuwa Mgeni Rasmi wetu Waziri wa Fedha Dk.Mwigulu Nchemba 
umewezesha kufikia mafanikio ya hatifungani hii kwa kiwango cha hali ya 
juu na kwa ufanisi mkubwa, kwani ulikuwa mgeni rasmi katika hafla ya 
uzinduzi wa mauzo ya hatifungani hiyo iliyofanyika Novemba, 4 mwaka 
2024.
“Na leo wewe ni Mgeni Rasmi katika hafla ya kuorodhesha 
hatifungani hii katika soko la hisa la Dar es Salaam (DSE).Tunakushukuru
 kwa kuwezesha mafanikio haya makubwa kwa kiwango cha hali ya juu.
“Mafanikio
 haya yana maana kubwa katika ustawi na maendeleo ya sekta ya fedha, 
kwani inaonesha imani waliyonayo wawekezaji kwa benki ya Azania na 
masoko ya mitaji, ambapo masoko ya mitaji hapa nchini yamekuwa na bidhaa
 mpya na bunifu zinazokidhi matakwa ya wawekezaji wa ndani na wa 
kimataifa,”amesema CPA.Mkam
Ameongeza
 kuwa mafanikio hayo ni uthibitisho wa mazingira wezeshi ya kisera, 
kisheria na kiutendaji yanayotolewa na Serikali ya Awamu ya Sita chini 
ya Uongozi madhubuti wa Rais Dkt. Samia Saluhu Hassan,akisaidiwa na 
Waziri wa Fedha kuisimamia Sekta ya Fedha.
Amefafanua baadhi ya 
mazingira hayo wezeshi ni uwepo wa vivutio vya kuwekeza katika masoko ya
 mitaji, ambapo katika mwaka wa Fedha 2021/2022, kupitia Sheria ya Fedha
 uliwezesha kuidhinishwa maombi ya kuweka kivutio cha kuwekeza katika 
hatifungani za kampuni na taasisi kwa kuondoa kodi ya zuio kwenye faida 
ya hatifungani za kampuni na taasisi. Hiyo imekuwa mojawapo ya vivutio 
kwa wawekezaji kwenye hatifungani ya Benki ya Azania.
Pia uwepo 
wa punguzo la kiwango cha chini chaushiriki katika uwekezaji kwenye 
hatifungani ya benki ya Azania, kilichoidhinishwa na CMSA kutoka 
shilingi milioni moja hadi Sh. 500,000). Punguzo hilo limewezesha 
ushiriki wa wawekezaji wengi, ikiwa ni pamoja na wawekezaji mmoja 
mmoja(retail investors) ikijumuisha makundi maalum, hususan vijana na 
wanawake.
Aidha ubunifu wa kuweka malipo ya riba ya hatifungani 
kwa wawekezaji kufanyika mara nne kwa mwaka badala ya mara mbili, ambapo
 CMSA imeidhinisha wawekezajikulipwa riba kila baada ya miezi mitatu 
(3)badala ya miezi sita (6).
“Hatua hii pia imekuwa kivutio 
kikubwa kwa wawekezaji, kwani inawezesha wawekezaji kuwa na ukwasi na 
kipato katika muda mfupi, na hivyo kuwezakukidhi mahitaji mengine.Poa 
elimu ya uwekezaji inayotolewa kwa umma na wadau katika sekta ya fedha 
kuhusu fursa na faida zinazopatikana katika masoko ya mitaji.”
CPA.Mkama
 amesema mafanikio ya hatifungani ya benki ya Azania ni hatua muhimu 
katika utekelezaji wa Mkakati wa Serikali wa kuwa na njia mbadala za 
upatikanaji wa rasilimali fedha kwa ajili ya kuendeleza na kukuza 
biashara; na kugharamia shughuli za maendeleo katika sekta ya umma na 
binafsi.
Amefafanua kuwa kama ilivyoelezwa kwenye taarifa ya 
Mkurugenzi Mtendaji; na kwenye Waraka wa Matarajio wa benki ya Azania, 
Fedha kupitia mauzo ya hatifungani hii zitatumika kutekeleza mkakati wa 
benki ya Azania wa kukuza na kuendeleza biashara, ikiwa ni pamoja na 
kutoa mikopo kwa kampuni ndogo na za kati za ujasiriamali (SMEs) ambazo 
zinatoa huduma katika sekta za uchumi; na ambazo zinatoa huduma kwa 
makundi ya wanawake na vijana.
Hivyo kwa mantiki hiyo hatifungani
 hiyo inawezesha utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Kuwezesha 
Upatikanaji wa Rasilimali Fedha kwa Kampuni Ndogo na za Kati za 
Ujasiriamali 2023/24 – 2028/29,
Ambapo kampuni ndogo na za kati 
za ujasiriamali (SMEs)ambazo ni kichocheo na kiungo muhimu katika sekta 
ya kilimo, viwanda na biashara zitafaidika na hivyo kuchagiza maendeleo 
na ustawi wa sekta ya fedha na uchumi kwa ujumla hapa nchini.
“Tunawapongeza
 sana Bodi na Menejimenti ya benki ya Azania kwa kuchukua hatua hii 
ambayo ni kichocheo muhimukatika maendeleo ya uchumi. Kuorodheshwa kwa 
Hatifungani ya Benki ya Azania katika Soko la Hisa leo hii, kunaongeza 
thamani ya uwekezaji katika Hatifungani za Kampuni na Taasisi kwa 
asilimia 8.17 na kufikia Shilingi bilioni 837.31, kutoka Shilingi 
bilioni 774.04.
“Hivyo, tuna kila sababu ya kuipongeza Bodi na 
Uongozi wa benki ya Azania; pamoja na taasisi na wataalamu wote 
walioshiriki katika kuwezesha mafanikio haya. Ninatambua kwamba, kazi 
hiyo haikuwa ndogo na rahisi lakini mmeweza kufanya kazi yenu vizuri na 
hivyo kufanikisha hatua hii kwa weledi na kwa ufanisi mkubwa.
“Natoa
 mwito kwa Benki zingine za Biashara, Taasisi za Fedha, kampuni binafsi 
na Mashirika ya Umma kutumia fursa zilizopo katika masoko ya mitaji kama
 ambavyo Benki ya Azania imetumia fursa ya kupata shilingi bilioni 63.27
 kupitia masoko ya mitaji kwa kuuza hatifungani.
“Mamlaka ya 
Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA)itaendelea kuweka mazingira wezeshi na
 shirikishi kwa ajili ya kuwezesha taasisi katika sekta ya umma na 
binafsi kupata rasilimali fedha kwa ajili ya utekelezaji wa mikakati 
yenye lengo la kujenga uchumi shindani kwa maendeleo ya watu.”
Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), akigonga kengele kuashiria kuorodhoreshwa rasmi kwa Hati Fungani ya Benki ya Azania ijulikanayo kama Bondi Yangu, katika Soko la Hisa la Dar es Salaam (DSE), Hafla iliyofanyika katika Ofisi za DSE, jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine aliziasa taasisi zingine kuiga mfano wa Azania Bank wa kujiorodhesha kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam na kutoa fursa kwa wananchi kushiriki kukuza uchumi wao binafsi na uchumi wa nchi kwa njia za kidijitali.
.jpeg)



 

.jpeg)


.jpeg)

.jpeg)











.jpg)



Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...